Loading ...

0
UjuziNet . 12th Jun, 2021

Una mtandao wa watu wenye hela?

Watu wote ambao hatuna mitaji, hela na wala hatukui kibiashara ni kwasababu moja kuu hatuna mtandao wa watu wenye hela.

 

Ukifungua simu yako,utakutana na namba za watu wa aina gani? Wana hela?

 

Kabla sijasema neno hapa ngoja kwanza nikupeleke kwenye familia za matajiri duniani. Familia kama Rockerfeller Family, Rothschild family…na nyingine duniani utakutana na tabia ambazo zimeridhishwa vizazi na vizazi. Ukikutana na familia masikini duniani utakutana na vijitabia vimerithishwa vizazi na vizazi….kutoka kwa babu, baba, mtoto na wajukuu na vitukuu huko.

 

 

Tukianza na hii familia ya Rockerfeller inafahamika duniani kibiashara. Ni familia ya kibiashara. Tukimfuatilia mjukuu David Rockerfeller alipokufa miaka ya hivi karibuni alikufa akiwa billionea na Zaidi alifahamika kama guru wa kukusanya mtandao wa watu wenye thamani ya mabilionea. Siri kubwa ya familia za kitajiri ni kuwa na mitandao ya watu wenye thamani ya mabilioni.

 

Mfano huyu David Rockerfeller alikuwa na zaidi ya namba mawasiliano za watu wakubwa na muhimu kwenye biashara zake zaidi ya 200,000. Yaani ni hivi alikuwa na business cards za watu muhimu duniani hasa wenye hela. Utaniuliza alizitunza wapi?

 

 

Kuna hii kitu inaitwa Rolodex ; ni kama file Fulani la kutunza kadi. Yaani huyu David huyu alikuwa na Rolodex yenye urefu wa futi 5 imetunza kadi za watu muhimu kwenye biashara zake; jaribu kufikiria wewe hapo una kadi ngapi or namba za watu muhimu wangapi wenye hela?


 

Kitu cha ajabu, ngoja nikuambie namna alivyokuwa anatunza kumbukumbu za hao watu muhimu kwenye biashara zake..yaani watu wenye hela… Kwenye kila kadi inaonyesha jina la huyo mtu, sekta gani yupo, biashara yake, muda mwingine hata utajiri wake, taarifa zake zikionyesha alioa lini, kama aliachana na mke or mume wake lini yaani alipeana talaka lini, mke wake ni nani, ana Watoto wangapi, mara ya kwanza walionana wapi, namba za simu, email zake, nini waliongea kwa mara ya mwisho…

 

Yaani ni kwamba ukichukua Rolodex yake ina thamani ya matrilioni ya pesa. Nikikuuliza Rolodex yako ina thamani ya shilingi ngapi? Au huna hata rolodex? Ukiona hadi picha ya hiyo kadi , inaonyesha ameonana na Donald Trump mwaka 1971 , akatunza kumbukumbu lini ameoa, lini alimtaliki mke wake sijui mwaka 90 na 93 akaoa tena yaani taarifa zote muhimu.

 

Unadhani Ray Croc aliweza vipi kupata wawekezaji kama si kwa kutumia mtandao wa watu wenye pesa aliokusanya na kutunza?

 

Yeyote yule ambaye ni Tajiri duniani, yeyote yule ambaye ni mwanasiasa mkubwa duniani ana rolodex yake yenye thamani ya matrillioni na atakuambia kuwa hakuna thamani kubwa duniani kibiashara kama thamani ya mtandao ulionao. Kama huna mtandao wenye thamani nakuhakikishia hata uwe na ndoto ya kuwa billionea sahau hii safari mpaka utakapoanza upya kuzalisha mtandao wenye thamani na kutengeneza rolodex yako yenye thamani ya mabilioni.

 

Rolodex yako inatakiwa iwe na thamani ya watu muhimu wafuatao;

 

a)    Watu wanaoweza kuwa chanzo cha mitaji ya biashara yako. Wewe unayelalamika kuwa sina mtaji si kwamba huna mtaji ila ni kwamba huna watu wa maana. Huna watu ambao unaweza kuwashirikisha na kuwashawishi kuhusu faida ya wao kuwekeza kwao. Hii haitokei kiajari ajari lazima uwakusanye hao watu ndani ya rolodex yako.

 

b)    Watu ambao wanaweza kuwa wanasheria wako. Wanaoweza kukusaidia pale unapohitaji msaada. Kuna dada mmoja alikuwa anataka muhuri tu wa mwanasheria kwenye biashara yake, akaenda kwa wanasheria wakamwambia laki mbili. Nikampa mawasiliano ya mwanasheria wangu akaenda kumpigia mhuri kwa Tshs elfu 10 kwasababu tu tunafahamiana na ni sehemu ya Rolodex yangu. Ni kama ndugu yangu. Wanasheria wanaoweza kukusaidia kwenye biashara, pale unapokutana na ishu


 

muhimu iwe kwenye real estate, umiliki wa kampuni, kodi na mengine mengi….

 

c)     Mtandao mwingine ni watu wanaofahamika kama Connector; connector ni watu wanaomfahamu kila mtu muhimu. Nina Rafiki yangu ambaye nikitaka namba ya mtu mkubwa Serikalini nitapata. Yaani una kitu chako lakini unatafuta mtu ambaye anafahamiana na watu wa aina mbalimbali basi ukiwa na connector Maisha yako yatapona.Hawa connectors wanaweza hata kukuunganisha na wateja wakubwa wa biashara yako. Wana database kubwaaaa ambayo ndiyo hii ya rolodex tunayoongelea.

 

d)    Watu walio kwenye vyombo vya habari. Lazima uwe na watu walio kwenye media,kwenye TV, radio, magazeti na hata wenye influence kwenye social media. Rolodex yako lazima ijaye watu wa aina hiyo.

 

e)     Watu wenye taarifa muhimu kuhusu sekta yako, iwe ni watafiti wanaojua sekta yako in and out…wanaweza kuwa watalaamu nk.

 

f)       Celebrities yaani watu maarufu, unatakiwa kuwa na watu maarufu iwe kwenye muziki, siasa, movie ..watu wenye sauti kubwa, watu ambao wanaweza kukupigia kampeni na mambo yako yakaenda.

 

g)    Wanasiasa. Hakikisha unafahamiana na wanasiasa, viongozi wakubwa wa Serikali. Kipindi cha nyuma wakati nina Chuo nilikuwa nawasiliana na Rais Kikwete na nilifahamiana naye akiwa kama waziri wa Mambo ya ndani. Spika wa Bunge, yaani walikuwa ndiyo watu muhimu walionipa hata sapoti ya kuniunganisha na Ruge pamoja na Joseph Kussaga.

 

h)     Watu wenye hela, watu wanaomiliki makampuni mbalimbali ambao unaweza kuwauzia bidhaa or huduma zako. Hapa ni database ya kufa mtu. Huwezi kuwa mjasiriamali au muuzaji halafu huna database ya watu ambao wana sifa kubwa ya kununua bidhaa zako kwa bei kubwa. Kama unauza sabuni basi hakikisha una wakurugenzi wa makampuni ya usafi. Kama unauza chakula basi uwe na rolodex imejaa wamiliki wa hoteli , kama unauza huduma nk…uwe na watu ambao hata ukiwaambia wakuunge mkono watakuja na kukupandisha juu. Nakuuliza tena, Rolodex yako imejaa akina nani?

 

i)        Watu  wenye  mwonekano  mzuri.  Namaanisha  watu  wenye  sura  nzuri.

 

Wanawake wenye sura nzuri, wanaume wenye sura nzuri nk… Najua hapa utanielewa vibaya…mimi sina tabia ya kuwa mnafiki hapa. Ukienda kwenye hoteli utakutana na watu wenye mwonekano mzuri. Ukienda kwenye ndege utakutana na watu wenye mwonekano mzuri. Watu hupenda kununua kwa watu wenye mwonekano mzuri. Nilipoanzisha kampuni ya Global Corporate Performance tulikuwa na mdada mwenye


 

sura nzuri sana simtaji jina lake akisoma ujumbe huu atanikumbuka. Huyu dada alikuwa akienda kuongea na wateja lazima lazima wateja wampe cheque ….biashara ilikuwa inaenda kwasababu ndogo unayoweza

 

kuidharau mwonekano mzuri humfanya mteja kushawishika Zaidi…japo si kwamba ndiyo kila kitu. Unaweza kuwaajiri or hata kuwatumia kwenye sherehe, or maonyesho nk…

 

10)    Mwisho kabisa, mentors…, washauri wa biashara yako. Wanaoweza kukuongoza na kukuambia ukweli hapa ulipofanya sipo. Hawa watu kitalaamu wanafahamika kama Sounding Boards. Hawa watu wanaweza kukushauri or hata kukupa maelekezo n ahata kukuongoza…kumbuka hawa mentors nao wana network kubwa wanaweza kuwa chanzo cha wewe kupata network kubwa ya kuifanya rolodex yako iwe na thamani

 

Hawa watu wote kwenye Rolodex wanaweza wasikusaidie chochote kama hutawafanya waone umuhimu wako kwao. Narudia tena, hao watu wote hutanufaika nao kama hutawafanya waone umuhimu wako kwao. Labda umekuja na namna ambayo unafanya biashara ambapo na wao wananufaika kwa namna moja au nyingine, au labda mnasali pamoja na mmejenga urafiki yaani kiimani na wanasimama na wewe kwasababu wanaona wewe ni sehemu moja. Nilipokuwa nafanya kazi na Shigongo kama Rafiki yangu, tulikuwa tunasali kanisa moja Word Alive. Waulize waliokuwa wanasali kanisa hilo Sinza watakuambia wengi walidhani Shigongo ni ndugu yangu or kaka yangu.

 

 

Mfano Haris Kapiga, kipindi anaanza kanisa lake nilikuwa kama muumini wake wa kwanza …tulikuwa wachache na hiyo ikawa sababu ya mimi kufanya naye vipindi vingi zamani kupitia temino ya clouds media ….kulikuwa bonding iliyokuwa inatukutanisha…

 

 

Wengine labda unaweza kujenga ukaribu kwasababu mnashabikia timu moja or mnaenda golf pamoja or mnaenda kwenye mpira pamoja or mnakutana sana kwenye mpira pamoja or kwenye maonyesho pamoja etc na unahakikisha mnafurahia pamoja…watu wa aina hii watasimama kukusapoti kwasababu mpo pamoja. Hautapata shida kabisa kuwashawishi au kuuza unachotaka kuuza kwao.


 

Wengine labda mpo Chama kimoja. Mnapambana pamoja. Huwezi kuwa upo upinzani halafu mtu unayetaka kuwa naye karibu ni waziri ambaye yupo CCM hamwezi kuchangamana, so kibiashara lazima uchague moja …unataka kutumia siasa kunufaika kibiashara au kudidimia kibiashara. Kwasababu hapa mtashirikiana pamoja kwenye chama, mtafanya kazi pamoja za chama na hata ikiwa ni mambo ya kibiashara ni rahisi mtu huyo kuwa msaada kwako. Wengine labda mnaweza kuwa ni mtandao wako na mkawa karibu kwasababu mna adui wa aina moja yaani common enemy…

 

 

Mwingine labda mmepitia changamoto pamoja, nakumbuka ukaribu tuliokuwa na Paul Mashauri kuna changamoto tulipiitia pamoja. Kipindi nilipopoteza Chuo changu ni kipindi alipopoteza kampuni zake za mwanzo ..so akawa ni mtu wa karibu kama familia mpaka leo.

 

 

Mwingine ni Rafiki wa Rafiki or Rafiki ambaye mnawasiliana naye. Nakuambia leo anza kukusanya watu muhimu kwenye Maisha yako na kuwasogeza karibu. Anza kuwakusanya iwe kuanzia kanisani, kwenye mikutano, misikitini nk…kusanya watu wa maana itakusaidia kuwashawishi kuuza au kuwashawishi kwa chochote unachotamani kufanya.

 

 

Kuwa na mawasiliano ya karibu na hao watu lakini usipende kuomba omba msaada kwao. Jenga ukaribu ambao wao pia watakuona ni wa muhimu kwao. Angalia ni kitu gani unaweza kuwafanyia nitakuambia katika sura inayofuata namna unaweza kuwafanya wakuunge mkono kwenye chochote unachotaka wafanye kwaajili yako,

 

 

Jifunze kutumia muda mwingi kuwa na watu wa muhimu kwenye Maisha yako, watu wenye hela , matajiri. Watu wanaopambana kwenda juu.

 

Haiwezekani ushinde na mtu asiye na hela eti kwasababu ni jirani yako or ndugu yako. Huwezi kuwa na hela kwa kushinda na watu masikini hata kama ni ndugu zako or rafiki zako or majirani zako.Hata ukinielewa vibaya potelea mbali. Siku nzima mnaongelea visivyozalisha hela, unategemea nini?


 

Lazima uwe karibu na watu wenye hela or watu muhimu niliowataja kwenye rolodex yako ili ufikiri kihelahela, utende kama mwenye hela, utembee kama mwenye hela, uwe ni mtu unayewaza au kufikiri kama wenye hela .. Kuliko kucheza mpira na vijana wa mtaani kwangu bora nikalipie michezo ya golf hata kama sijui kucheza nikae karibu na wenye hela nijenge undugu or urafiki na kubeba kadi zao za biashara.

 

Kama huna watu hakuna biashara. Kama huna watu hakuna kanisa. Kama huna watu hakuna misikiti. Kama huna watu hakuna vyama vya siasa. Ukiingia kwenye sanaa ya kuuza ujue kwamba umeingia kwenye kazi ya kutengeneza mtandao na watu muhimu. Wewe unayekesha unazalisha bidhaa wakati huna watu, kama bidhaa zako unazozalisha ni sabuni utaoga mwenyewe na majirani wawili watatu na hutafika kokote…

 

 

Unapoenda kanisani nenda kasali ukue kiroho lakini usisahau kuzalisha watu wa kujaza kwenye rolodex yako.

 

Unapoenda msikitini nenda kwaajili ya ibada na kiroho lakini usisahau kuzalisha watu wa kujaza kwenye rolodex yako.

 

Unapoenda mpirani usiende tu kushangilia simba na yanga, nenda kakutane na watu wa kujaza kwenye rolodex yako,

 

Unapoenda kwenye maonyesho usiende tu kuonyesha bidhaa bali nenda kakutane na watu muhimu wa kujaza kwenye rolodex yako,

 

Unapoenda kwenye msiba usiende tu kuomboleza nenda kakutane na watu wa kujaza kwenye rolodex yako….Kuna Rafiki yangu nilimwambia aende



 

kwenye msiba badala yangu, msiba wa Mengi…na nikamsihi sana nenda ukaomboleze lakini usisahau kukusanya watu wa kujaza kwenye rolodex yako, nilipoenda kwenye msiba wa Ali Mufuruki nilienda kumuomboleza mentor na mwalimu wangu lakini pia nilienda na kukusanya watu wa kujaza kwenye rolodex yangu.


JIFUNZE ZAIDI HAPA


Shopping Cart

Loading...